Na Rose Jackson, ARUSHA,TANZANIA
MSIMAMIZI wa kundi la muziki la Contagious lenye makazi yake jijini Arusha,Njara Rasolomanana maarufu kama Dady amevamiwa na kundi la majambazi nyumbani kwake Kimandulo jijini hapa ambapo alijeruhiwa na kisha kuporwa vitu mbalimbali vyevye thamani ya kiasi cha zaidi ya
sh,12 milioni.
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita majira ya saa 1.30 asubuhi ambapo kundi la majambazi 17 wakitumia jiwe aina ya fatuma walivunja mlango wake na kisha kumjeruhi kabla ya kumpora vitu mbalimbali.
Akihojiwa na gazeti hili huku akionyesha majeraha katika eneo la uso na mgongo ke,Rasolomanana alisema kwamba wezi hao walifanikiwa kumpora simu tano,kompyuta ndogo tatu,na kiasi cha sh,4 milioni.
Njara ,ambaye ni raia wa Madagascar alisema kwamba tayari ameshafungua jalada la tukio hilo katika kituo kikuu cha polisi cha kati jijini Arusha na kupewa nambari za AR|RB|7548|2012 .
Kamanda mkuu wa jeshi la polisi mkoani Arusha,Liberatus Sabas alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kwamba jeshi lake bado linafuatilia kwa kina tukio hilo kwa lengo la kuwashikilia watuhumiwa.
Home »
» MAJAMBAZI YAMPORA SH. MILIONI 12, MKIONGOZI WA KUNDI LA MUZIKI ARUSHA
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !