Headlines News :
Home » » MICHUANO YA NETIBOLI TAIFA YAANZA, MTEMVU APANIA TEMEKE IENDELEE KULISHILIKIA KOMBE

MICHUANO YA NETIBOLI TAIFA YAANZA, MTEMVU APANIA TEMEKE IENDELEE KULISHILIKIA KOMBE

Written By Bashir Nkoromo on Saturday, December 28, 2013 | 11:57 PM

 Wachezaji wa timu ya Netiboli ya Temeke, wakiwa na mfadhili wa timu hiyo.Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu kabla ya timu tiyo kuchuana jana na timu ya Katavi katika mechi ya fungua dimba ya  michuano ya Netiboli Kombe la Taifa, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
DAR ES SALAAM, TANZANIA
KATIKA kuiwezesha timu ya netibali ya Mkoa wa Temeke kuendelea kubaki na kombe la ubingwa  ililolinyakua katika mashindano yaliyopita ya mprira huo Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, ameahidi kuisaidia timu hiyo kwa hali na mali.

Akizungumza wakati wa kuwakabidhi fedha za kijikimu kwa wachezaji wa timu hiyo, mwishoni mwa wiki katika ofisi yake, Mtemvu alisema yeye kama mdau wa michezo atahakikisha kombe hilo linabaki.

Katika hafla hiyo Mtemvu aliwakabidhi kiasi cha sh. 600,000 kama fedha za kujikumu kwa siku mbili kwanza na kuongeza kwamba atakuwa akifanya hadi pale mshindano hayo yatakapofikia tamati Januari 17, mwakani.

Kwa upande wake Nahodha wa timu hiyo,Malarena Muhagama, alisema, kama timu wamejipanga vilivyo kuhakikisha wanaendelea kuwa washindi katika mashindano hayo.

Muhagama alisema hilo linawezekana kabisa ukizingatia kwamba zaidi ya nusu ya wachezaji wao wanachezea timu ya taifa ya netiball.

Pia lisema katika kuhakikisha wanakuwa imara wakati wote wamekuwa wakifanya mazoezi kila siku na hivyo kuwaweka tayari wakati wote kukabiliana na timu shindani.

Kocha wa timu hiyo, Amina Musa, aliwataka mashabiki wa temeke kujijitokeza kwa wingi kuishangalia timu hiyo ambayo jana  ilifungua mashindano na timu ya Katavi na kuibuka na ushindi wa mabao 48 kwa 15.
 Mtemvu akisalimiana na wachezaji mbalimbali kabla ya michuano hiyo kuanza jana
 Mchezaji wa timu ya  Temeke Sekela Mwakanyuki (kulia) akitafuta njia ya kumpenya mchezaji wa Katavi Rose Ezrael, katika mechi hiyo  jana.
 Mchezaji wa Katavi akijaribu kuumiliki mpira
 Mchezaji wa TMK akimdhibiti mchewzaji wa Katavi asaipate bao langoni
 Hekaheka katikati ya uwanja wakati  wa mechi hiyo
Mchezaji wa Temeke akipachika bao golini mwa Katavi. Katika mechi hiyo Temeke iliibuka mshindi kwa mabao 58-27
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template