Headlines News :
Home » » MSHINDI 'MO KIDS GOT TALENT 2013' APATIKANA, NI MOREEN JULIUS

MSHINDI 'MO KIDS GOT TALENT 2013' APATIKANA, NI MOREEN JULIUS

Written By Bashir Nkoromo on Monday, December 30, 2013 | 6:21 AM

DSC_0018
Kijana Salum Nyangumwe (17) mshindi wa
 pili aliyeimba wimbo wa My Number One
 wa Msanii Nasib Abdul a.k.a Diamond wakati
 wa fainali za kusaka kipaji cha SUPA STAA 
wa watoto na vijana! la ”MO Kids Got Talent 2013"
 lililofanyika mwishoni mwa Juma kwenye 
Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach
 jijini Dar es Salaam.
Na.Mwandishi wetu.
Mtoto Moureen Julius(12), amejinyakulia
 kitita cha shilingi Milioni tano katika fainali
 za Shindano la “MO KIDS GOT TALENT 2013”
 lililofanyika kwenye hoteli ya Ledger Plaza Bahari beach lililoanza tarehe 25 hadi tarehe 28 mwezi huu ambapo fainali zilifanyika.
Shindano hilo lilijumuisha watoto zaidi ya mia mbili ambapo kila mmoja alijipatia nafasi ya kuonesha kipaji chake vikiwemo kuogelea, kuimba, kucheza, karate na vingine vingi.
Watoto 15 walichuana katika nusu fainali na kuchujwa hadi kufikia watoto watano na mwisho wa siku kupatikana SUPA STAA Moureen Julius aliyewafunika wenzake kwa kipaji alichonacho.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutangazwa mshindi wa kwanza aliyejinyakulia kitita cha sh.millioni tano, Mtoto Moureen Julius alisema pesa hizo alizoshinda atazitumia kwa kulipia ada na vifaa vingine vya shule.
Shindano hili la "MO KIDS GOT TALENT 2013" liliandaliwa na Frost Africa na kudhaminiwa na Mohammed Enterprises Tanzania Ltd. (MeTL) Group.
DSC_0030
Supa Staa wa Shindano la "MO Kids Got Talent 2013" Moureen Julius (12) akionyesha kipaji chake cha kucheza kwenye fainali za shindano hilo.
DSC_0039
Pichani juu na chini washiriki wa shindano la "MO Kids Got Talent 2013" wakiendelea kuonyesha vipaji vyao wakati wa fainali za shindano hilo.
4
Mtoto mwenye kipaji cha kuimba na kucheza.
DSC_0026
Jaji Hidaya Njaidi akitoa maoni yake kwa washiriki (hawapo pichani) waliokuwa wakichuana kuwani Shilingi Milioni 5 za Kitanzania zilizotolewa zawadi na Kampuni ya MeTL Group.
DSC_0070
Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko ambao ndio waandaji wa mashindano hayo na Meneja Masoko Msaidizi wa MeTL Group, Bw. Aunali Bandali (kulia) wakifuatilia kwa umakini mashindano hayo yaliyomalizika mwishoni mwa Juma.
DSC_0051
Jaji Mkuu wa shindano la "MO Kids Got Talent 2013" Salma Mziray akitoa maoni yake kwa washiriki waliofanikiwa kuingia tano bora.
DSC_0138
Pichani Juu na chini ni baadhi ya washiriki waliofanikiw kuingia tano bora wakionyesha manjonjo yao kwa mara nyingine tena kabla ya kutajwa mshindi wa shilingi Milioni tano kutoka Kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd. MeTL Group lilifanyika mwishoni mwa Juma kwenye Hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach jijini Dar.
DSC_0177 DSC_0186 DSC_0206
Jaji Kiongozi wa shindano la "MO Kids Got Talent 2013" akiteta jambo na Raisi wa wanafunzi, Allan Lucky a.k.a SKONGA kabla ya kutangaza mshindi.
DSC_0210
Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Jaffer na Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko wakionekana kufurahishwa na vipaji vya watoto hao.
DSC_0228
DSC_0245
Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko, akitoa nasaha kwa washiriki walioingia tano bora ambapo amewata wazazi kuhakikisha wanaendeleza vipaji vya watoto.
DSC_0248
Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Jaffer, akiwapongeza vijana walioingia tano bora.
DSC_0332
Tano Bora wakiwa na matumbo joto.
DSC_0253
Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Jaffer, akitoa nasaha zake ambapo amesema mashindano haya yatakuwa yakifanyika kila mwaka nchini lengo ni kuibua vipaji vya watoto na vijana.
DSC_0340
Mshindi wa tano Gloria Collin (10), akipokea maboksi ya zawadi zilizotolewa na kampuni ya Mohammed Enterprises Tanzania Ltd (MeTL) kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko ambao ndio waandaji wa mashindano hayo.
DSC_0355
Mshindi wa nne Lisa Deogratius (17) naye alipkeza zawadi mbalimbali kutoka kampuni ya MeTL.
DSC_0378
Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Jaffer, akiwausia washiriki ambao mmoja kati ya hao ataibuka mshindi wa kitita cha shilingi milioni tano kutoka MeTL Group.
DSC_0393
Jaji Kiongozi wa shindano la "MO Kids Got Talent 2013" Salma Mziray akitoa shukrani kwa kampuni ya MeTL kwa kuweza kuibua vipaji vya watoto na vijana.
DSC_0405
Na mshindi niiiiiiiiiiiii.....!!!! Raisi wa wanafunzi, Allan Lucky a.k.a SKONGA akitangaza mshindi.
DSC_0406
Mtoto Moureen Julius (12) akilia kwa furaha baada ya kuibuka mshindi.
DSC_0414
Kilio cha furaha kwa Moureen Julius.
DSC_0416
Wow.....!!!...Hongera Mwanangu.
DSC_0427
Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Jaffer, akikabidhi kitita cha Shilingi Milioni tano za Kitanzania kwa Supa Staa wa Shindano la "MO Kids Got Talent 2013" Moureen Julius (12). Wanaoshuhudia tukio hilo ni baba mzazi wa Moureen pamoja na Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko ambao ndio waandaji wa shindano hilo.
DSC_0435
Afisa Mtendaji Mkuu wa Frost Africa, Bw. Peter Sekasiko, akiwa ameongozana na Supa Staa wa Shindano la "MO Kids Got Talent 2013" Moureen Julius (12) huku nyuma yao wakiwa na ulinzi mkali kuelekea kuzungumza na waandishi wa habari.
DSC_0457
Supa Staa wa Shindano la "MO Kids Got Talent 2013" Moureen Julius (12), akifanya mahojiano na waandishi wa habari. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Masoko wa MeTL Group, Bi. Fatema Jaffer.
DSC_0110
Sehemu ya watoto, wazazi/walezi waliohudhuria fainali za shindano la "MO Kids Got Talent 2013" lililofanyika mwishoni mwa juma kwenye hoteli ya Ledger Plaza Bahari Beach.
DSC_0056
DSC_0195
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria hafla hiyo.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template