Headlines News :
Home » » UCHAGUZU MKUU TASWA KUFANYIKA FEBRUARI 16 MWAKA HUU

UCHAGUZU MKUU TASWA KUFANYIKA FEBRUARI 16 MWAKA HUU

Written By Bashir Nkoromo on Wednesday, January 29, 2014 | 4:23 AM

AMIR MHANDO
UCHAGUZI Mkuu wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), utafanyika Februari 16 mwaka huu jijini Dar es Salaam kama ulivyopangwa na Kamati ya Utendaji ya chama.
 
Hata hivyo sekretarieti ya TASWA imekubaliana kusogeza mbele muda wa kulipia ada kwa wanachama hadi Jumanne Februari 4 mwaka huu, badala ya Ijumaa Januari 31, 2014 iliyokuwa imepangwa awali, lengo likiwa ni kuwezesha wanachama wengi zaidi kulipia ada zao ili waweze kushiriki uchaguzi huo.
 
Wanachama wote walioshiriki uchaguzi wa mwaka 2007 ama 2010 au Mkutano Mkuu wa mwaka 2012 wana sifa ya kushiriki uchaguzi huo wanachotakiwa kufanya ni kulipia ada zao kuanzia mwaka 2011.
 
Malipo yafanywe kwa Mhazini Msaidizi, Mohammed Mkangara, 0658-123082 na hakuna mwanachama mpya atakayekubaliwa kujiunga na chama kwa sasa mpaka baada ya Uchaguzi Mkuu.
 
Nawasisitiza wanachama kuhakikisha wanatumia vizuri muda uliobaki kwa kulipia ada zao ili waweze kushiriki mkutano huo. Kamati ya Uchaguzi ya TASWA inatarajiwa kukutana Jumatatu ijayo kuzungumzia mambo mbalimbali yahusiyo uchaguzi huo.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template