Headlines News :
Home » » WABUNIFU 'LADY IN RED' FEBRUARI 14, MWAKA HUU HADHARANI

WABUNIFU 'LADY IN RED' FEBRUARI 14, MWAKA HUU HADHARANI

Written By Bashir Nkoromo on Monday, February 10, 2014 | 10:59 AM

*Wamo  magwiji: Ally Remutulla, Mustapha Hassanal, Khadija Mwanamboka, Martin Kadinda
*Chipukizi wamo  Faustin Simon, Water Edward,Willex Willibard,  Jackson, Alabama King
Na Andrew Chale
WABUNIFU mbali mbali watakaopamba miaka 10 ya onyesho la mavazi lijulikanalo kama ‘Lady in red Super brand, 10th Anniversary’ linalotarajiwa kufanyika Februari 14, tayari majina yao yamewekwa hadharani. Onyesho la mwaka huu linatarajia kufanyika kwenye hoteli ya Serena, jijini Dar es salaam, Februari 14, huku asilimia ya mapato ya fedha hizo zinatarajia kusaidia wathirika wa dawa za kulevya wa kituo cha Kikale Kilichopo Mkoani Pwani.
 
Akizungumza na wandishi wa habari  leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Fabak Fashions inayoandaa onyesho hilo, Asia Idarous Khamsin (pichani), alisema kila mwaka onyesho hilo huja kitofauti ikiwemo kuongeza vionjo mbalimbali katika kufikia mafanikio kwenye tasnia ya ubunifu  na mitindo ya mavazi hapa nchini.
 
“Safari hii, steji ya Lady in red’, inatimiza miaka 10, huku ikijivunia kuibua vipaji vya wabunifu wengi hapa nchini, na wengine kwa sasa wanamajina makubwa kwenye yasnia hiyo, hivyo tutaendelea kutoa nafasi kwa wabunifu chipukizi mara kwa mara ilikufikia malengo yao” alisema Asia Idarous.
 
Asia Idarous aliwataja wabunifu magwiji watakaopamba steji hiyo kuwa ni pamoja na Khadija Mwanamboka, Mustapher Hasanal , Ally Remtulla, Lucky Creation, Martin Kadinda, Ghymkana Hilali,  Paka wear, Gabriel Molel, Fransiska Frankoo,  Shirima, Salim Ally, Ameed Abdul, Mgese Makory, Kiki Collection, Rose fashion, Diana Magesa, Rio Paul na wengine.
 
Kwa upande wa wabunifu chipukizi watakaopamba ni pamoja na Faustin Simon, Water Edward, Brian Hango, Benedict Mnzava,Crissiwelly Uissoson,Willex Willibard,  Jackson, Gumbala, Jabir Jumanne, Alabama King, Agusta Masaki, Nelson Tomas, Bebi Juliet Mtandu, Ummi fashion/Ummi Investiment Comapany, Asmahan Eva, Hassan Nasor, Juniper Mafuru, Ante Ngongi, Adam Hassan, Jaquline, Kijangwa na Waiz Shelukindo.
 
Aidha, Asia Idarous aliongeza kuwa, kwenye onyesho hilo, pia kutakuwa na burudani mbalimbali ikiwemo kutoka bendi ya Babloom Trio na Mwanamuziki mahiri wa nyimbo na ngoma za asili, Wanne Star. Katika onyesho hilo ambalo litafanyika siku hiyo ya Februari 14, ambayo pia itakuwa ni siku ya Wapendanao ‘Valentine’s Day’ , kiingilio kitakuwa sh 30,000 kwa viti vya kawaida huku viti maalum ikiwa sh 50,000.
 
Tayari tiketi za onyesho hilo zimeanza kuuzwa ikiwemo vituo vya duka la Fabak fashion, lililopo mikocheni mkabala na kituo cha Mwalimu Nyerere huku kwenye hoteli ya Serena, zikipatikana mapokezi.
 
Kwa upande wa wadhamini wakuu wa shindano hilo ni pamoja na kinywaji cha Zanzi pamoja na kampuni ya nywele ya Darling. Wengine ni CXC, Times fm, Clouds media, Vijimambo blog, michuzi media group, channel ten, Elite Computer, Eventlites, One touch-solution, Raysa Style, Paka Wear, Dj Bula, Magic fm, DTV, Jambo Leo, I View media, Vayle Spring, Voice of American na wengine wengi.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template