Headlines News :
Home » » SAYANSI YA SOKA: UJUMBE KWA YANGA, SIMBA NA AZAM

SAYANSI YA SOKA: UJUMBE KWA YANGA, SIMBA NA AZAM

Written By Bashir Nkoromo on Friday, September 30, 2016 | 7:41 AM

0713682040,0767682041

Makala hii inalenga kutoa mafunzo muhimu ya dhana juu ya utafiti wa hivi karibuni juu ya Sayansi ya Soka na matumizi ya mazoezi madogomadogo (Multiple Small Sided Games) katika kubaini, kuendeleza vipaji vya vijana wanaochipukia kutika soka kwa kutimia elimu mwendo kwa binadamu (Human Kinetics) ili kupata mafanikio katika soka la dunia ya leo.

Ni ukweli usiopingika kuwa changamoto ya ushambuliaji dhidi ya Ulinzi bado inaendelea (Jay Miller: 2014) hususani nchini Tanzania, katika makala hii tutabaini stadi, ufundi na mbinu muhimu za Kisayansi za kuvunja mipango iliyoratibiwa ya ulinzi katika soka.  Ili timu yeyote iweze kufanya mashambulizi yenye mafanikio inapaswa kutengeneza fursa kwenye theluthi ya ushambuliaji (John Hackeworth: 2014) kam umoja na uwili(One Twos),mchezo wa kupishana(Overlap),Pasi Jozi(Double Pass),Ufungaji wa magoli 4 kwa kukimbia(Four Goal shooting on the Run),muungano wa wachezaji watatu kufunga(Three Man Combinations to Goal),Mchezo wa magoli 3 na faida ya ongezekeo la namba(Three Goal Numerical Advantage Gama),Upishanaji wa kufunga(Ovelapping to score) Mpito(3v2 to 4v3 Transition) na Ruwaza ya Goli(Pattern Play to Goal). 

Ni muhimu kutumia uchezaji wa Kimuungano (Combination Play) ambao unaweza kusababisha umaliziaji na ufungaji wa kisayansi (Finishing and Shooting) kwa kutumia mbinu zifutazo za uchezaji wa kimuungano kama Ukaguzi kabla ya ndege kupaa(Check in),Uchukuzi wa kisigino(Heel Takeover), uchukuzi mshazali(Staight Takeover), kupitiliza(Overlap) na Zunguka uso kimbia(Round the face Run).

Ili timu yeyote iweze kuwa na falsafa na mkakati wa mashambulizi wenye mafanikio sharti washambulie kupitia pembezoni (Dean Wurzberger: 2014) kwa kutumia mazoezi kama;kikosi cha kupiga mipira ya mkato na umaliziaji (Squad scrossing and Finishing),Rajua ya upitilizaji wa wachezaji watatu (Three Player Overlap Pattern),Umalizaiaji wa mielekeo mitatu(Two direction finishing),Mipira ya Mkato na umaliziiaji katika theluthi ya mwisho, mchezo wa wiga 8v8(8v8 Winges Game), Mbawa huru za kupigia mipira ya mkato(Free Wing Crossing Boxes) ,Uchezaji wenye manufaa wa pembezoni (Functioal Flank Play),Mashambulizi ya pembezoni ya wachezaji 9 dhidi ya 9 (9v9 Flank Attack) kama jinsi ambavyo timu za Simba na Yanga zinavyotegemewa kufanya kwa kawaida, vinginevyo kwa kuzingatia falsafa ya umiliki wa mpira falsafa na mkakati wa ushambuliaji unaweza kupitia katika theluthi ya kati (Ken Lolla: 2014) kwa kutumia mazoezi kamaUmiliki kuelekea malengo(Possession to Targets),Mtafute mshambuliaje uende naye(Find The Forrward nd Go),Mchezo wa magoli mengi(Multiple Goal Game),Mchezo wa Magoli sita(Six Goal Game),Funga ndani ya dakika % Ushinde(Score in Five To Survive), kama ambavyo timu za Azam na Simba ambavyo hutarajiwa kucheza.  Wakati mwingine mashambulizi huweza kufanyika kutoka theluthi ya ulinzi (Mike Noonan: 2014) kwa kutumia mazoezi kama;pass mruko na uzungushaji wa mpira (Skip pass and ball Rotation),Hatua za mwanzo wa ujenzi wa ushambuliaji kutoka nyuma (GK+5v3 to 3v5+GK) ,mwelekeo wa pembezonikushambulia(Advancing the Wingbacks to Attack),Uvunjaji wa msongo wachezaji 9 dhidi ya 6(9v6 Breaking Pressure) na Mashambulizi ya wachezaji  Kumi(Ten Attacks) kama ambavyo timu za Simba na Yanga zinavyotarajiwa kucheza.

Walakini timu vyingi hazina Stadi, Mbinu na Ufundi wa kutosha kuelewa na kutumia michezo midogomidogo ya kurudiwa, kwata na mazoezi (Multiple Small Sided Games and Drills) ili kuanzisha kuratibu na kutenda mashambulizi ya kisayansi nchini.  Hata mazoezi ya kupasha yanayofanyika kabla ya mechi kuanza kueleza hualisia huu kwa kuzingatia mawanda ya udukuzi katika soka (Soccer Intelligence) (Dick Bate & Ian Jeffreys: 2015).

Mfululizo wa makala hii  unalenga kuonyesha uhitaji mkubwa uliopo na pengo lililopo nchini katika kufundisha Sayansi ya Soka na hususani Elimu Mwendo Binadamu (EMB) yaani (Human Kinetics).  Mwandishi wa mada hii na wadau wengine wa sayansi ya soka wanalenga kuanzisha Chuo cha Sayansi ya soka hapa nchini.  

Hivi sasa wapo katika hatua za mwisho za kuandaa mitaala na kupitia mchakato wa Usajili wa Chuo hicho ili kutatua tatizo hili ambalo linachagia kudidimiza soka la Tanzania. 

Makala hii pia inalenga kufanya uoni (Observation) wa kisayansi katika viwango vya matumizi ya michezo midogomidogo ya kurudiarudia na kwata (multiple small sided games and drills) za sayansi ya soka la ushambuliaji na falsafa zake katika timu 3 kubwa za Tanzania ambazo ni Simba, Yanga na Azam wakati wa ligi kuu mwaka 2016/2017.  

Lengo la makala hizi ni kuzijengea uwezo timu hizi kuona umuhimu wa walimu, wachezaji, wachambuzi, wawekezaji katika soka, wadhamini wa soka, watangazaji wasoka, wabashiri wa soka, watazamaji wa soka na wapenzi wa soka kuelewa soka la kisayansi na kuliendeleza soka la Tanzania kisayansi.  Aidha timu nyingine za ligi kuu, na madaraja mengine ya kwanza, pili, tatu na nne kitaifa, kimikoa, kiwilaya yataweza pia kulielewa soka la kisayansi kwa lugha rahisi ya Kiswahili.  

Makala hii inalenga pia kujenga uwezo wa vijana wanaochipukia wenye vipaji vya soka ili waweze kuelewa na kutumia stadi, mbinu na ufundi wa kisayansi ili kuendeleza vipaji vyao hata kama wanaelimu ya kiwango kidogo kwa kutumia stadi, mbinu na ufundi wa elimu mwendo binadamu (Humana Kinetics).  Ayumkini tutaweza kuendeleza soka la Tanzania.

Nilipomuhoji mmoja wa wanagunzi wa Chuo cha soka cha Elimu mwendo  wa binadamu (Human Kinetics Academy) Stanford Andambike ambaye ni mshambuliaji (Striker) juu ya mehci ya Simba na Azam alikuwa na haya ya kusema.

Japokuwa mchezaji Shiza Kichuya aliyefunga goli, yeye alinukuliwa kusema na vyombo vya habari kuwa “Kocha aliniambia nipige shitu nje ya kumi na nane”.

Mwanafunzi Stanford Andambike kutoka Human Kinetics Academy alisema “Simba wametumia falsafa ya wachezaji wote kushambulia wote kulinda na soka la mguso mmoja kwa mfumo wa 4:4:2. Yawezekana alisema hivyo kwa vile hiyo ndiyo falsafa inayosisitizwa kule chuo cha Human Kinetics Academy.  

Tuseme hapa bayana kuwa mfumo huu unafaida ya timu kujibana (Compact) ila unapaswa kuwa yabisi (solid) katikati na unawawezesha viungo kuwasaidia walinzi na washambuliaji kwa urahisi.  Faida yake kubwa ni kwamba ni mfumo rahisi maranyingi kubadili katika 4-4-2 kwenda kwenye mfumo wa ushambuliaji zaidi wa 4-2-4 au hat 4-3-3 bila kuwa na uharibifu kwa wachezaji au mahitaji ya kubadilisha wachezaji.  

Ni mfumo unaofaa kwa kuwaruhusu wachezaji wa viungo kuwasaidia washambuliaji na walinzi (Patrick Morgan: 2006).  Tuseme bila  kigugumizi kuwa mfumo kama 4-3-3 ambayo hubadilika na kuwa 4-5-1 wakati wa ulinzi na 4-4-2 ambao hubadilika na kuwa 4-4-1-1 wakati wa ulinzi mshambuliaji akichukua nafasi ya kiungoni wakati mwingine timu hucheza zaidi  na kiungo kuliko 5-1-4 kwenye nusu yao ya uwanja wanapojilinda na katika jaribio la kuzuia bunduki kubwa, mifumo hii kwa sasa siyo muhimu sana kwa malengo iliyobuniwa kuyatekeleza.  

Mameneja wengi duniani wa Timu huamini kuwa dhana ya mifumo washambuliaji wanavyohusika na kupaswa kutenda ni mifumo inayokufa taratibu.  Nafasi ya mifumo hii sasa inachukuliwa na washambuliaji 6 ambao wanaweza kubadilishana nafasi wakati wakusaidiwa na mabeki wa kushoto(full backs0 katika soka la kileo kuna mifumo mipya inayotokana na mapinduzi ya soka la ushambuliaji (Revolution in attacking football).  Beki wa kushoto (full baks) leo ndio wachezaji muhimu katika kikosi cha mashambulizi na wanaotizamwa zaidi katika timu (The Secret Footballer’s Guide to the modern Game, page 158).  Kwa mantiki hiyo mimi naziangalia timu zetu kwa kuwaangalia Malika Ndeule (Simba), Haji Mwinyi (Young Africans sc), Bruce Kangwa (Azam Fc) na kwa soka la Tanzania lijalo kwa kazi nzuri ya Serengetii Boys namwangalia Nickson Clement Kibabage na uwezo wao katika stadi, mbinu na ufundi wa Kisayansi.

Kuna mifumo mingi ya kileo kama; 4-2-3-1 katika mfumo huu (fullbacks) wote wawili wanaweza kwenda mbele muda mmoja na timu inaweza kushambulia mara moja kwa kutumia wachezaji hadi 8.  Sharti wachezaji na viungo waratibiwe pande zote.  

Hapo kuwa mfumo huu unatishio la mashambulizi ya kushitukiza (counter attack) pembeni chini.  Aidha (fullbacks) sharti wawe imara kwani pia hutakiwa kucheza kama winga.  Mfumo huu unatishio la kuathiriwa na timu yenye washambulizi imara wa kati.

Katika mfumo wa 3-5-2 wachezaji winga (winbacks) ndio muhimu katika mafanikio ya mfumo huu.  Kifo cha mfumo wa 4-4-2 kimesababisha kuzaliwa kwa zama mpya za mikakati na mifumo katika soka.

Kuna baadhi ya wachambuzi wanahusisha zama hizi na kifo cha winga.  Nafasi zao zinachukuliwa na fullbacks na viungo washambuliaji wenye vipaji.  Hawa hupeleka mipira pembeni.  Kuondoka kwa winga kunafanya fullbacks waweze kushiriki katika ushambuliaji wanapojisikia, leo mashambulizi mengi yanaanzishwa na fullbacks na ndio wachezaji timamu zaidi katika timu.  

Dunia imeshuhudia timu ya Manchester United wakimsainisha mkataba kijana wa miaka 18 kutoka Southapton kwa paundi milioni 30 akivunja rekodi ya vijana wanaochipukia. 

Mwanafunzi Stanford Andambike aliendelea kusema kuwa pia Simba walikuwa wanashambulia kupitia winga hususani Ibrahim Ajib.  Na pia Simba wametengeneza fursa za kufunga kupitia kucheza umoja uwili (0ne-Twos) Shiza Kichuya na Ibrahim Ajib na Laudit Marugo na Ibrahim Ajib.

Kwa maelezo yake pia wamecheza uchezaji wa kimuungano wa umaliziaji na upigaji shuti (Finishing and Shooting) uchukuzi mnyofu (Straight Takeover) kati ya Ibrahim Ajib na Shabalala .

Joseph Omog ambaye ni Coach wa Simba, Jackson Mayanja ambaye ni Kocha msaidizi, Technical Advisor Hassan Selemani na Mussa Hassani Mgosi ambaye ni meneja  wa timu wanafahamu kuwa walipanga kufanya nini zaidi.  Wanafahamu falsafa, mfumo na mikakati waliyoipanga na kutekeleza hata itakayotumika tarehe 1 Oktoba 2016 dhidi yon a watani wao wa jadi Yanga.

Aidha kwa upande wa Azam kocha Zeben Harnandes na msaidizi wake Yeray Romero na mshauri wao wa ufundi Pablo Borge sambamba na meneja wao Simon Alando wanajua  falsafa waliyolenga kutumia na mkakati waliojiwekea na mfumo husika.

Aidha kama tulivyokwisha sema hapo awali mfumo waliotumia Azam wa 3-5-2 unategemea sana wingbacks ili uwe na mafanikio.  Beki mfagizi (Sweeper) kwa maana hiyo Himid Mao pekee ndiye alitarajiwa kuwa bila msongo na mpira.  Hatuna uhakika kama Azam hucheza na Mfagizi (Sweeper).  

Japokuwa mfumo huu hubadilika na kuwa 4-1-4-1 na hii hutokea wakati timu hucheza na mshambuliaji mmoja na namba 10 ambaye alipaswa kuwa Shaban Chilunda.  Wengi hutizama mfumo huu kama njia ya kuhifadhi nguvu kwenye mechi kwani wachezaji wachezao kwenye kiwango cha juu cha uchezaji wao ni winga na nyma (wingbacks) ambao mara nyingi hushambulia.  Kama tulivyokwisha sema fullbacks siku hizi ndio wingbacks ambao hupasha kuwa timamu kuliko wachezaji wote uwanjani.  Ikimaanisha kuwa beki wako (center half) hawapendi kwenda pembeni (wide curves) kulind kwani hufanya ………….. …

Kuna mengi unapaswa kutumia waachezaji ulionao kutumia mfuno unao iwezesha timu kucheza vizuri.  Ukweli ni kwamba kwa kutumia mfumo wa 3-5-2 ni rahisi kufanya mshambulizi ya kushtukiza kama timu itakaa nyuma na kusahau hatari ya wingback.  Timu ikiamua kucheza kasi ya mchezaji huwa rasilimali kubwa ya mfumo kama Arjen Robben wa spain                                                                     
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template