LONDON, England
Bondia wa ngumi za ridhaa, Mtanzania Seleman Kidunda, kesho Jumapili anapanda ulingoni kuanza kupeperusha bendera ya taifa kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyozinduliwa juzi Ijumaa jijini London.
Kidunda, 28, ambaye ni bondia pekee kupata tiketi ya kucheza mashindano hayo katika mchezo wa ngumi za ridhaa nchini, anapanda ulingoni kuumana na Belous Vasilii, 23 raia wa Moldova.
Mshindi kati ya Kidunda na Vasilii, atakuwa na kazi ya ziada wakati atakapotakiwa kupanda tena ulingoni hapo Agosti 3, kuzipiga na Shelest Yuk wa Ukraine, ambaye yeye ameingia hatua ya pili kutokana na ubora wake.
Pambano kati ya Kidunda na Vasilii ambalo ni la uzzito wa Kilo 69, upande wa wanaume, litatanguliwa na mapambano mengine 12 ya ngumi leo.
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !