Headlines News :
Home » » PAMBANO LA YANGA, RUVU SHOOTING LAINGIZA SH. MILIONI 47

PAMBANO LA YANGA, RUVU SHOOTING LAINGIZA SH. MILIONI 47

Written By Bashir Nkoromo on Sunday, October 21, 2012 | 9:35 AM


*SERENGETI BOYS YAINGIA KAMBINI
*AFRICAN LYON YAONYWA
DAR ES SALAAM, TANZANIA
Pambano la Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Ruvu Shooting lililochezwa jana (Oktoba 20 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa wenyeji Yanga kushinda mabao 3-2 limeingiza sh. 47,615,000.


Watazamaji 8,233 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo iliyochezwa kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000, na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 8,420,578.47 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 7,263,305.08.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni posho ya msimamizi wa kituo sh. 120,000, kamishna wa mechi sh. 203,000, waamuzi sh. 381,000, mwamuzi wa akiba sh. 70,000, usafi na ulinzi wa uwanja sh. 2,350,000 na Wachina (stadium technical support) sh. 2,000,000.

Umeme sh. 300,000, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000, ulinzi wa mechi sh. 3,500,000 wakati tiketi ni sh. 2,959,100. Gharama za mchezo sh. 2,806,859.49, uwanja sh. 2,806,859.49, Kamati ya Ligi sh. 2,806,859.49, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 1,684,115.69 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,122,743.80.

SERENGETI BOYS

Kikosi cha wachezaji 25 wa timu ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys) kimeingia kambini leo (Oktoba 21 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kujiandaa kwa mechi ya raundi ya mwisho ya michuano ya Afrika kwa vijana.

Serengeti Boys ambayo iko chini ya Kocha Jakob Michelsen itacheza mechi hiyo ya raundi ya tatu na mshindi kati ya Congo Brazzaville na Zimbabwe ambapo tayari Congo Brazzaville imefanikiwa kupata ushindi wa ugenini wa mabao 2-1. Mechi ya marudiano itachezwa jijini Brazzaville kati ya Oktoba 26-28 mwaka huu.

Katika mechi hiyo ya raundi ya tatu, Serengeti Boys itaanzia nyumbani katika mchezo utakaofanyika Novemba 17 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, wakati mechi ya marudiano itachezwa wiki mbili baadaye.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) liko katika mikakati ya kuhakikisha Serengeti Boys inapata mechi mbili za kirafiki za kimataifa kabla ya kumvaa mshindi kati ya Congo Brazzaville na Zimbabwe. Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 zitafanyika Machi mwakani nchini Morocco.

AFRICAN LYON YAONYWA
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imeipa onyo kali timu ya African Lyon kutokana na washabiki wake kuweka bango lililoandikwa ‘We believe in 0777’ kwenye mechi yake dhidi ya Azam iliyochezwa Oktoba 6 mwaka huu Uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.

Bango hilo ambalo si la mdhamini wa Ligi Kuu ya Vodacom halitakiwi kuonekana tena kwenye mechi ambazo African Lyon inacheza vinginevyo Kamati ya Ligi itachukua hatua kali dhidi ya timu hiyo.

Kamati ya Ligi imezikumbusha timu zote zinazoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom kuzingatia kanuni zinazotawala ligi hiyo ili iweze kuendeshwa kwa ufanisi.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template