Kamati
ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu cha Wanawake (TWFA) imetangaza kipindi
cha pingamizi kwa waombaji uongozi katika uchaguzi wa chama hicho utakaofanyika
mwezi ujao.
Kwa
mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati hiyo Ombeni Zavala, kipindi cha pingamizi ni
kuanzia Oktoba 5 hadi 9 mwaka huu, na pingamizi ziwasilishwe ofisi za TWFA.
Mwisho wa kupokea pingamizi ni saa 10 kamili jioni, na hakuna ada kwa ajili ya
pingamizi.
Pia
amesema usaili kwa wagombea utafanyika kati ya Oktoba 12 na 14 mwaka huu
kuanzia saa 3 asubuhi kwenye ofisi za TWFA zilizopo Uwanja wa Kumbukumbu ya
Karume, Dar es Salaam. Kila mgombea anatakiwa kufika kwenye usaili akiwa na
vyeti vyake halisi (original) vya kitaaluma.
Waombaji
wa uongozi kwenye uchaguzi huo ni Lina Paul Kessy, Isabellah Hussein Kapera na
Joan Ndaambuyo Minja (Mwenyekiti) wakati mwombaji wa nafasi ya Makamu
Mwenyekiti ni Roseleen Kissiwa.
Nafasi
ya Katibu Mkuu imevutia wagombea wawili; Amina Ali Karuma na Cecilia Oreste
Makafu. Mark Raghton Mhango ni mgombea pekee wa nafasi ya Katibu Msaidizi kama
ilivyo kwa Rose Msamila anayewania nafasi ya Mhazini.
Wagombea
wanne wameomba nafasi ya ujumbe wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF). Wagombea hao ni Furaha Emily Francis, Zena Suleiman Chande,
Jasmin Badar Soud, Juliet Edwin Mndeme. Wanaowania ujumbe wa Kamati ya Utendaji
ni Rahim Salum Maguza, Triphonia Ludovick Temba na Sophia James Charles.
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !