Headlines News :
Home » » ALIYECHEZESHA SIMBA NA SHANTI KUCHEZESHA LIBOLO

ALIYECHEZESHA SIMBA NA SHANTI KUCHEZESHA LIBOLO

Written By Bashir Nkoromo on Saturday, March 2, 2013 | 8:24 AM


KWANZA, SUL, Angola
MWAMUZI Nhleko Simanga Pritchard kutoka nchini Swaziland ambaye alichezesha mechi baina ya Wekundu wa Msimbazi na Al Ahly Shandi ya Sudan mwaka jana, ndiye atakayechezesha mechi ya kesho dhidi ya Libolo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyopatikana kutoka Chama cha Soka cha Angola leo asubuhi, mwamuzi huyo atasaidiwa na na wenzake Mkhabela Bhekisizwe, Mbingo Petros na Fabudze Mbongiseni ambão wote wanatoka Swaziland.

Kati ya hao, ni Nhleko na Petros pekee ambão ndiyo waliochezesha mechi ya Shandi ambayo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 yaliyofungwa na Haruna Moshi (77), Patrick Mafisango ambaye sasa ni marehemu (88) na Emmanuel Okwi (90).

Wachezaji wote hao watatu waliofunga katika pambano hilo hawatacheza katika mechi ya Libolo kwa sababu tofauti. Mafisango alifariki kwa ajali siku mbili baada ya kurejea kutoka Sudan kwenye mechi ya marudiano ambako Simba ilitolewa.

Okwi amehamia katika klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia na Boban ameshindwa kusafiri na timu kwenda Angola kwa sababu ya kushikwa na malaria kali.

Kamisaa wa pambano hilo lililopangwa kuanza majira ya saa tisa kamili kwa saa za hapa (sawa na saa 11 jioni kwa saa za Tanzania) anatarajiwa kuwa Mandla Mazibuko kutoka nchini Afrika Kusini.

Libolo yatumia uwanja kutafuta ushindi
Mwandishi Wetu, Angola
BENCHI la ufundi la Simba SC jana limeukagua Uwanja wa Estadio Libolo itakakochezwa mechi ya kesho ya Ligi ya Mabingwa Ulaya baina ya Wekundu na Libolo na kubaini siri nzito.

Vipimo vya Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Liewig, vilibaini kwamba uwanja huo una upungufu wa takribani mita sita kwa urefu na upana kulinganisha na viwanja vingi vya soka.

Kwa mujibu wa Liewig, uwanja huo umepunguzwa ukubwa ili kusaidia timu ya Libolo ambayo inafahamika sana kwa kufunga mabao mengi ya mipira iliyokufa (adhabu, kurusha n.k).

“Kutokana na hali hii, maana yake ni kwamba kila itakapokuja kona, itakuwa hatari kwa sababu kuna umbali mdogo kutoka kwenye kona hadi goli. Itakuwa hatari hivyohivyo kwenye mipira ya kurusha na ya adhabu. Ni muhimu tumeliona hili mapema,” alisema.

Alisema atawaeleza wachezaji wake kujiepusha kutoa kona au mipira ya kurusha bila ya sababu kwa vile inaonekana hiyo ndiyo silaha kubwa ya wapinzani hao wa Simba.

“Kama unakumbuka, hata goli lao la Dar lilitokana na mpira wa kurusha halafu ikapigwa krosi. Ndiyo maana nafikiri wameleta mechi hii huku badala ya Luanda ili watumie faida hii vizuri,” alisema.

Nchini England, Uwanja wa Britannia unaotumiwa na timu ya Stoke City inayocheza Ligi Kuu ya nchi hiyo unafahamika pia kwa kuwa mdogo kwenye eneo la kuchezea kuliko viwanja vingi vya nchi hiyo.

Hata hivyo, inaelezwa kwamba lengo kuu la kuuweka uwanja huo katika eneo hilo ni kutumia nguvu ya mipira ya kurusha na adhabu nyingine ambayo ndiyo silaha kubwa ya Stoke. Miaka miwili iliyopita, robô ya magoli yaliyokuwa yakifungwa na timu hiyo yalitokana na mipira ya kurusha ya Rory Delap
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template