Headlines News :
Home » » NAPE: KILA LA KHERI TAIFA STARS

NAPE: KILA LA KHERI TAIFA STARS

Written By Bashir Nkoromo on Saturday, June 8, 2013 | 7:56 AM

Nape Nnauye, Katibu wa NEC, Itikadi/Uenezi CCM
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeitakia kila la kheri timu ya Taifa, Taifa Stars katika mechi yake na Timu ya Taifa ya Morocco ya kutafuta tiketi ya kucheza kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil.

Akizungumza kutoka Dar es salaam ,Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesema CCM inaitakia kila la kheri na mafanikio katika mchezo huo wa kesho na kwamba CCM inatambua umuhimu wa taifa Stars kushinda mechi hiyo.


"Naamini dua  za CCM na Watanzania wote kwa jumla zinaweza kuiwezesha Taifa Stars  kushinda mechi hiyo ambayo ni muhimu sana, Watanzania tunaomba muiombee Taifa Stars, tunaimani nayo, bila shaka itashinda kesho" alisisitiza Nape
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template