Headlines News :
Home » » MISS TANZANIA AAGWA RASMI NA WAZIRI, AAHIDI KUTAFUNA MFUPA ULIOMSHINDA FISI, ASEMA ATAREJEA NA TAJI LA DUNIA

MISS TANZANIA AAGWA RASMI NA WAZIRI, AAHIDI KUTAFUNA MFUPA ULIOMSHINDA FISI, ASEMA ATAREJEA NA TAJI LA DUNIA

Written By Bashir Nkoromo on Friday, August 30, 2013 | 7:28 AM

Waziri wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dr Fenela Mukangara (kulia) akimkabidhi Bendera ya Taifa Mwakilishi wa Tanzania katika mashindano ya Urembo ya Dunia, Redd's Miss Tanzania Briggiter Wilfred kulia ikiwa ni ishara ya kutambua wajibu wake kwa kipindi chote cha mashindano hayo nchini Indobesia, Kushoto ni Mkurugenzi wa LINO AGENCY Hashim Lundenga. 

Na Mwandishi Wetu

REDD’S Miss Tanzania, Brigitte Alfred amedai atahakikisha anatwaa taji la dunia (Miss World), ambalo litafanyika Septemba 28 huko Indonesia.


Akizungumza wakati akiagwa katika hafla iliyofanyika kwenye hoteli ya Giraffe iliyopo Kunduchi, Dar es Salaam, Brigitte alisema nia yake kubwa ni kushindana na si kuwa msindikizaji.


“Nina uhakika mkubwa wa kutwaa taji hilo, kwani vigezo vyote ninavyo na nimejiandaa kwa muda mrefu mno,” alisema Brigitte.


Mrembo huyo ambaye anatarajiwa kuondoka Jumatatu kwenda Indonesia alisema, Kamati ya Miss Tanzania imemsaidia kwa kiasi kikubwa, hivyo ni matarajio yake atatwaa taji hilo.


“Niseme wazi nimejiandaa kwa muda mrefu mno na nashukuru wote walionisaidia kwa njia moja au nyingine na hii inanipa moyo wa kufanya vizuri zaidi,” alisema.


Naye Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenella Mukangara aliyekuwa mgeni rasmi, wakati akimkabidhi bendera ya taifa alimtaka ahakikishe anaipeperusha vizuri na kufanya vyema katika mashindano hayo.


“Fahamu fika kwamba unakwenda Indonesia kama Miss Tanzania na si Brigitte, hivyo unatuwakilisha Watanzania wote, sisi tuko nyuma yako unachotakiwa ni kujiamini tu na utafanikiwa.”


Mrembo huyo alifanikiwa kulitwaa taji la Redd’s Miss Tanzania mwishoni mwa mwaka jana, akitokea kitongoji cha Sinza na Kanda ya Kinondoni.


Redd’s Miss Tanzania kwa sasa inadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template