Headlines News :
Home » » MPAMBANO WA ISHA MASHAUZI, MALKIA LEYLA ULIKUWA ‘BALAA’!

MPAMBANO WA ISHA MASHAUZI, MALKIA LEYLA ULIKUWA ‘BALAA’!

Written By Bashir Nkoromo on Monday, October 24, 2016 | 3:55 AM

dar-live1
Kabla ya mpambano Abubakari Soud ‘Amigo’ wa Jahazi alipanda jukwaani kuwanogesha mashabiki.
dar-live2
Mtangazaji wa Redio Times FM, Aisha Mbegu (kulia) akirusha sarafu ili kumpata mwanamuziki wa kuanza kukamua kati ya Leyla na Isha. Kushoto ni mshereheshaji MC wa Jahazi, Mwasity Robert, na katikati ni mwakilishi wa Isha na Leyla.
dar-live3
Baada ya Isha kuanza kukamua shabiki huyu alikunwa na hivyo kuvamia jukwaa kwenda kumtunza.
dar-live4
Sehemu ya umati uliofurika ukumbini hapo kufuatilia mpambano huo.
dar-live5
Leyla akifanya yake baada kupanda jukwaani.
dar-live6
Mtangazaji na MC wa shughuli hiyo, Aisha Mbegu wa Redio Times FM, uzalendo ulimshinda na kuanza kubanjuka.
dar-live7
Wanenguaji wa Jahazi wakimsindikiza Leyla.
dar-live8
Leyla akiwanogesha mashabiki.
dar-live9
Isha Mashauzi aliyevamia tena jukwaa akiwa katika na vazi jingine.
dar-live10
Isha na kundi lake wakishambulia jukwaa.
dar-live11
Wakati Isha akipagawisha mashabiki, Leyla alikunwa na kumvamia Isha jukwaani na kumtunza hali iliyosababisha mayowe ya kushangilia.
dar-live12
Uhasama wao ulikuwa ni jukwaani tu, kwani baada ya kushuka jukwaani wote walikuwa kitu kimoja.

MASHABIKI wa burudani, hususan muziki wa taarab, usiku wa kuamkia jana walipata burudani ya aina yake wakati wakali wa muziki huo, Isha Mashauzi na kundi lake la Mashauzi Classic kwa upande mmoja na Leyla Rashid kwa upande mwingine akiwa na kundi lake la Jahazi Modern Taarab, walipotoana kijasho kwenye onesho maalum la kutaka kujua nani mkali kati yao.

Kabla ya mpambano huo kulikuwa na ubishani mkali kwa mashabiki ambapo upande fulani ulisema Isha ndiye mkali kuliko Leyla huku wengine wakisema “aaah, wapi bwana Leyla ndiyo mkali zaidi; pale Isha haingii hata kwa nini”!

Hatma ya ubishi huo ni mpambano uliowakutanisha wawili hao na kuwaacha mashabiki wakijionea na kuamua wenyewe. Kabla ya wakali hao kupanda jukwaani mshereheshaji wa shughuli hiyo, Aisha Mbegu, wa Redio Times ilibidi arushe sarafu hewani ili kumpata mwanamuziki wa kuanza kulivamia jukwaa maana walianza kutegeana. Baada ya sarafu kurushwa Isha ndiye aliyeangukiwa na zali la kuanza kuonesha mavitu vyake jukwaani.
(PICHA/HABARI: RICHARD BUKOS /GPL)
Share this article :

1 comment:

  1. Thanks for sharing, nice post! Post really provice useful information!

    Công ty vận chuyển hàng nước ngoài FadoExpress hàng đầu chuyên vận chuyển, chuyển phát nhanh siêu tốc đi khắp thế giới, nổi bật là dịch vụ gửi hàng đi mỹ, gửi hàng đi nhậtgửi hàng đi đài loan và dịch vụ chuyển phát nhanh đi hàn quốc uy tín, giá rẻ

    ReplyDelete

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template