Headlines News :
Home » » TFF YAPONGEZA UONGOZI MPYA SHIREFA

TFF YAPONGEZA UONGOZI MPYA SHIREFA

Written By Bashir Nkoromo on Monday, October 29, 2012 | 1:44 PM


DAR ES SALAAM, TANZANIA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatoa pongezi kwa uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Shinyanga (SHIREFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika juzi (Oktoba 27 mwaka huu).

Ushindi waliopata viongozi waliochaguliwa kuongoza chama hicho unaonesha jinsi wajumbe wa Mkutano Mkuu wa SHIREFA walivyo na imani kubwa kwao katika kusimamia mchezo huo mkoani Shinyanga.

TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya SHIREFA ambayo imechaguliwa chini ya uenyekiti wa Benester Lugora.

Uongozi huo mpya una changamoto nyingi, kubwa ikiwa ni kuhakikisha unaendesha shughuli za mpira wa miguu Shinyanga kwa kuzingatia katiba ya SHIREFA pamoja na vyombo vya mpira wa miguu vilivyo juu yake.

Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya SHIREFA na Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa kuhakikisha uchaguzi huo unaendeshwa kwa mujibu wa Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.

Viongozi waliochaguliwa ni Benester Lugora (Mwenyekiti), Nassoro Said (Katibu Mkuu), Bivin Kapufi (Katibu Msaidizi), Mbasha Matutu (Mjumbe wa Mkutano Mkuu TFF) na Michael Kaijage (Mwakilishi wa Klabu TFF).
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template