Headlines News :
Home » » ALBINUS AWA MFALME WA UZITO WA UNYOYA WA DUNIA KWA VIJANA

ALBINUS AWA MFALME WA UZITO WA UNYOYA WA DUNIA KWA VIJANA

Written By Bashir Nkoromo on Saturday, March 30, 2013 | 4:53 AM

 DAR ES SALAAM, Tanzania.
Albinu Felesianu wa Namibia leo ameudhihirishia ulimwengu kuwa yeye kweli ndiye Mfalme wa uzito wa unyoya duniani kwa vijana baada ya kumgalagaza bondia Herbert Quartey wa Ghana katika mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa Windhoek Country Club Resort  and Casino leo tarehe 29, March 2013.

Umati wa watu wasiopungua elfu 20 walijazana katika ukumbi huo wa burudani wakimshangilia kwa nderemo na vifijo bondia wao Albinus wakati alipokuwa anafanya vitu vyake kwenye ulingo.
Baada ya mtangazaji wa ulingo kutamka kuwa “Na sasa bingwa mpya wa uzito wa unyoya duniani kwa vijana ni Albinus Felesianu” mayowe ya wapenzi wa ngumi waliojazana katika ukumbi huo yaliweza kusikika kilometa tatu mpaka katikati ya jiji la Windhoek.
Hata hivyo, haikuwa kazi rahisi kwa Albinus kuunyakua mkanda wa ubingwa wa dunia kwa vijana kwani Mghana Herbert Quartey naye alikuwa mbogo kwani alirusha kila aina ya masumbwi yaliyomo kwenye kitabu.
Wawili hao walichapana makonde mazito kama watu wenye uzito mkubwa na kama sio uwezo na ujuzi wa referii Deon Dwarte wa Afrika ya Kusini kazi ingekuwa ngumu sana kwani kila bondia alijaribu kumpata mwenzake katika sehemu zinazoumiza ili kuumaliza mpambano mapema lakini ujuzi na ubishi wa kila mmoja ulifanya kusiweko na knockout yoyote!
Hii ni mara ya kwanza kwa nchi ya Namibia kuweza kuandaa mpambano wa ubingwa wa dunia wa IBF na wakali hao waliweza kuufanya umati wote uliohudhuria kulipuka kwa makelele ya kushangilia kila wakati.
Alikuweko Harry Simon, ambaye ndiye Mnamibia aliyeweza kuufanya mchezo wa ngumi kupendwa na kuwa maarufu sana nchini humu. Uwezo na utukutu wa Harry Simon ulingoni umeufanya mchezo wa ngumi kupendwa karibu na kila Mnamibia.
Walikuweko pia wageni wengine wengi lakini kampuni ya simu ya Telecom ambayo ndio waliokuwa wadhamini wa mpambano huo imejikusanya kila aina ya sifa na upendo kutoka kwa wananchi wa Namibia jinsi inavyo dhamini mchezo wa ngumi!
Mpambano huu uliandaliwa na Kinda Nangolo wa kampuni ya Kinda Boxing Promotions ambayo ndio waandaaji wa mpambano ujao wa mwezi wa Mei wa bingwa wa IBF Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki ya Kati katika uzito wa unyoya bondia Gottlieb Ndokosho. Mpambano wa IBF wa Kimataifa wa bondia Harry Simon nao utafanyika mwezi wa Juni.
Aidha, Immanuel “Prince’ Naidjala”wa Namibia na Lesley Sekotswe wa Botswana watarudiana tena mwezi wa July kumpata bingwa wa kimataifa wa uzito wa bantam baada ya kutoka sare walipokitana wiki iliyopota nchini Namibia.
Share this article :

0 comments:

Speak up your mind

Tell us what you're thinking... !

Total Pageviews

Comments

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Proudly powered by Blogger
Copyright © 2011. theNkoromo SPORTS - All Rights Reserved
Template Design by Creating Website Published by Mas Template